ADVERTISE WITH US

Fahamu zaidi kuhusu Google Pixel 2 na Google Pixel 2 XL , Simu mpya kutoka Google.

Google hivi karibuni waliingiza sokoni matoleo yao mapya ya simu za Google Pixel 2 na Pixel 2 XL  ikiwa ni muendelezo wa toleo la Google Pixel na Pixel XL yaliyotoka mwaka jana. Sasa nakuchambulia machache ambayo unaweza kukutana nayo pindi utakapo kuwa tayari kununua simu hii.

  • MUONEKANO 
Simu hizi zina muonekano mzuri na wa kipekee, Google wameamua kuifanya iwe simu simple, ikiwa material ya Aluminium lakini ukiishika unaweza kusema kuwa imeundwa kwa plastiki, Google wamejaribu kuifanya simu iweze kushikwa vizuri kwa kuongeza material ya plastiki lakini ukweli ndiyo huo imeundwa kwa Aluminium.

  • YALIYOMO KWENYE SIMU HIZI. 
Simu hizi zinakuja zikiwa na Specifications bomba kwani zinatumia Processor ya Qualcomm Snapdragon 835 kama kwenye Samsung Galaxy S8, zinakuja zikiwa na Ram ya 4GB, uhifadhi wa ndani wa 64GB, kwenye upande wa betri kuna mabadiliko kwani PIXEL 2 ina ukubwa wa betri la 2700 MAH, na PIXEL 2 XL ina ukubwa wa betri 3520 MAH.
Google Pixel 2 ina kioo chenye ukubwa wa inch 5 na Google Pixel 2 XL ina kioo cha ukubwa inch 6, na zote zinatumia teknolojia ya Gorilla Glass.

  • CAMERA 
Hii ndiyo sehemu ambayo watu wengi wamekuwa wakifatilia sana, na hapa Google Pixel 2 na Pixel 2 XL wamefanya vizuri japokuwa hizi simu zote hazina Camera mbili kwa nyuma (Dual Camera) kama yalivyo matoleo mengi simu janja siku hizi badala yake kuna kinaitwa Dual Pixel kwenye Camera.
Google Pixel 2 na Pixel 2 XL zote zimewekwa Processor maalum kwa ajili ya picha hivyo kuifanya simu hii kuwa nzuri sana kwenye kupiga picha.

Simu zote hizi zina 12-MegaPixel dual-pixel nyuma na Camera ya mbele ina 8-MegaPixel.
Tizama picha zilizopigwa na hizi simu hapa. 

  • AI na MFUMO WA UENDESHAJI. 
Ninapo zungumzia AI nazungumzia Artifical Intelligence na tunazungumzia Google Assistant, unaweza kutumia msaidizi wa Google kuiamrisha simu yako kufanya kile unachotaka kama kupiga simu, kutuma SMS na mengine, jambo lingine jipya ni ACTIVE EDGE teknolojia mpya ambayo inakuwezesha kubinya simu yako ili uweze kutumia Google Assistant, utalazimika kuset Active Edge kwenye simu yako ili uweze kutumia.

 Active Edge.

Simu hizi zinatumia mfumo wa uendeshaji wa Android 8.0 (Oreo)
Hayo ni machache nimekugusia kuhusu simu hizi mbili, jambo lingine la kufahamu ni bei ya simu hizi, Google Pixel 2 inaanza kuuzwa kwa dola za kimarekani $649, na Google Pixel 2 XL inaanza kuuzwa kwa $849

No comments: