Rais wa Chad, Idriss Deby ameondoka jijini Dar es Salaam kuelekea nchini kwake. Alisindikizwa kwenye uwanja wa ndege wa JKIA na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Rais huyo aliwasili nchini kwa ziara kikazi ya siku 2 akiwa na mkewe Mama Hinda Deby na alipokelewa na mwenyeji wake Rais Magufuli na kisha kulakiwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa na wananchi.
Rais Magufuli alifanya mazungumzo na Rais Idriss Deby Itno Ikulu Jijini Dar es Salaam.



SOURCE BY: +Bongo5 TV
PICHA: OFISI YA WAZIRI MKUU



No comments:
Post a Comment